Mwanamuziki
maarufu wa miondoko ya nyimbo laini duniani maarufu kama Blues, mwanamama
Celine Dion ameamua kusitisha ziara yake ya bara la Asia kutokana na Maradhi ya
Mumewe
Mwanamuziki
huyo mwenye umri wa miaka 46 amejisogeza karibu zaidi kwa wanadani wake René
Angélil (72) anayekabiliwa na maradhi ya Cancer inayomtesa kwa kipindi kirefu
sasa
Celine,
ameamua kuwa karibu na mumewe zaidi katika kipindi hiki akidai kuwa ni kipindi
kigumu na chenye msongo wa mawazo kwake, kutokana na maradhi yanayomsibu mumewe
(Rene) kutokana na tumor iliyotolewa kooni mwake Mwezi Disemba, mwaka jana
Amebadilisha
tarehe za ziara ya Asia, zinazotarajiwa kuanza Novemba 11 huko Nagoya, Japan. Alipangiwa
kuanza ya Las Vegas mnamo Ijumaa hii lakini ameipotezea pia.
“Ninataka
kuchangia kila chembe ya nguvu zangu kwa kupona kwa mume wangu, na kufanikisha
hilo, ni muhimu kwa mimi kuutumia muda huu kwa ajili yake na watoto wetu.” Aelezea
kadamnasi. “Na pia nawaomba radhi
mashabiki zangu woote popote mlipo, kwa yaliyotokea. Nawashukuru pia kwa
ushirikiano mkubwa na mapenzi ya dhati”
Inasemekana kuwa
mapumziko hayo yatamnufaisha Celine pia ambaye amekuwa akisumbuliwa na maradhi
ya Uvimbe kwenye misuli ya koo
Hii ni mara
ya pili kwa Rene kukabiliana na Cancer baada ya kwanza kutibiwa mwaka 1999, na
Celine ameonesha hali chanya kuhusu kutibika kwa mumewe pindi alipohojiwa Julai
Mwaka huu
“Maisha
huamurisha baadhi ya vitu kwako, lakini anaendelea vizuri sana. Anafanya kazi
kwa bidii, na amekuwa mtiifu sana, kitu ambacho si rahisi kwake. Hivyo, ni
mtiifu, mchapakazi, anacheza na watoto na anafurahi pia” asema Celine.
Mwanadada
huyo wa muziki wa taratibu alifunga ndoa na mwenzi wake mwaka 1994 baada ya
kuonana kwa mara ya kwanza mwaka 1980. Kwa pamoja, wana watoto watatu wa kiume;
Rene-Charles na mapacha wawili (Eddy na Nelson)
No comments:
Post a Comment